KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 9, 2015

IVORY COAST MABINGWA WAPYA AFRIKA


IVORY Coast jana iliibuka kuwa mabingwa wapya wa soka barani Afrika baada ya kuichapa Ghana kwa penalti 9-8 katika mechi ya fainali iliyochezwa mjini Malabo, Equatorial Guinea.

Mshindi wa pambano hilo ilibidi apatikane kwa njia ya penalti tano tano baada ya timu hizo kumaliza dakika 120 zikiwa suluhu.

Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Ivory Coast kutwaa taji hilo tangu 1992, ilipoishinda Ghana kwa staili hiyo hiyo ya penalti tano tano.

Kipa Boubacar Barry aliibuka shujaa wa Ivory Coast baada ya kufunga penalti ya mwisho na kisha kuokoa shuti la kipa mwenzake wa Ghana, Razak Braimah.

Pambano hilo lilikuwa na ushindani mkali kutokana na timu zote mbili kucheza kwa kasi na
nguvu, kila moja ikipania kutoka uwanjani na ushindi.

No comments:

Post a Comment