KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, February 14, 2015

STAND UNITED YAIFANYIZIA MGAMBO SHOOTING



TIMU ya Stand United imeichapa mabao 4-1 Mgambo Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Kambarage Shinyanga.

Ushindi huo unakuja siku chache baada ya wachezaji wa timu hiyo kupewa mafundisho na kocha Msaidizi wa timu ya taifa ya Uholanzi, Patrick Kluivert.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Barcelona alizuru Shinyanga wiki hii kufungua cha soka cha watoto katika sekondari ya Com na akapata fursa ya kuhudhuria mazoezi ya Stand United Uwanja wa Kambarage na kuwapa mawaidha

Katika mechi nyingine za Ligi Kuu, Mbeya City imelazimishwa sare ya bila kufungana na wenyeji Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati Mtibwa Sugar nayo imetoka 0-0 na wenyeji Ndanda, Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.

No comments:

Post a Comment