KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, February 10, 2015

BARCELONA NAO KUTUA BONGO, KUCHEZA NA MAGWIJI WA BONGO


KIKOSI cha magwiji wa Barcelona kitazuru Dar es Salaa Machi 28 mwaka huu kwa ajili ya mchezo mmoja wa kirafiki dhidi ya wachezaji nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, maarufu Tanzania Eleven.

Almasi Kasongo, Mwenyekiti wa Chama cha Soka Dar es Salaam, wanaoandaa ziara hiyo kwa ushirikiano na kampuni ya Prime Time Promotions amesema hayo leo katika Mkutano na Waandishi wa Habari ukumbi wa City Sports Lounge, Dar es Salaam.

Mkutano huo, ulihudhuriwa na mkali wa zamani wa mabao wa Barcelona, Mholanzi Patrick Kluviert ambaye amethibitisha ujio wa nyota waliotaka Camp Nou miaka ya nyuma kidogo.

Ziara hiyo ni matunda ya ziara ya magwiji wa wapinzani wa Barcelona, Real Madrid Agosti mwaka jana, ambao pia walicheza na magwiji wa Tanzania na kushinda 3-1 Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment