KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 26, 2015

NASRY KUJIUNGA NA ASPIRE FOOTBALL DREAM SENEGAL



Kijana Nasry Daudi Aziz aliyezaliwa Agosti 21, 2001 amechaguliwa kujiunga na kituo cha kukuza vipaji cha Aspire Football Dream kilichopo katika mji wa Dakar nchini Senegal.

Mradi wa  Aspire nchini ulianza mchakato wa kusaka vijana mwezi Machi - Mei, 2014 ambapo vijana wengi walijitokeza na kuchaguliwa vijana 14 ambao walikwenda katika mchujo mwingine uliofanyika nchini Uganda uliowashirikisha vijana zaidi ya 50.

Kijana huyo ni miongoni mwa wachezaji 17 waliochaguliwa kati ya vijana 34 walikuwepo nchini Senegal kwa muda wa mwezi mmoja, ambapo kulikuwa na vijana wengi kutoka nchi mbalimbali barani Afrika na Amerika ya Kusini.

Kituo cha Aspire kilichopo Dakar nchini Senegal ni miongoni mwa vituo viwili vinavyoongozwa na mtoto wa mfalme wa Qatar na timu ya Barcelona, kituo kingine kipo mjini Doha.

Nasry Daud Aziz anatarajiwa kuondoka nchini Februari 28 mwaka huu kuelekea Dakar ambapo atakua kwenye kituo hicho kwa mkataba wa miaka miatano.

 Kutoka nchini Tanzania Nasry anakua ni kijana wa tatu kujiunga na kituo hicho, wengine ni Matine Taganzi na Orgenes Morrel ambaye aliitwa kwenye timu ya Taifa Stars maboresho na kocha Mart Nooj.

STAND NA SIMBA ZAINGIZA MIL 31, MBEYA CITY, YANGA MIL 74
Mchezo uliokuwatanisha wenyeji timu ya Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga dhidi ya timu ya Simba umeingiza jumla ya tsh. milioni 31.

Juma la watazamaji 5,439 waliingia uwanjani kushuhudia mchezo huo, ambao timu ya Stand imepata mgao wa tsh. 6,564,268.22 na Simba wakipata mgao wa tsh. 4,661,581.78.

VAT (18%) tshs. 4,763,135.59 huku FA  mkoa wakipata tsh.665,940.25, FDF tsh. 1,141,611.86, Bodi ya Ligi tsh. 1,522,149.15, Gharama za mchezo tsh. 1,617,283.47, Uwanja tsh. 2,854,029.66, Gharama ya tiketi tsh. 1,593,000,00, FDF tsh. 2,921,000.00, TFF tsh.2,921,000.00

Katika uwanja wa Sokoine mbeya jumla ya tsh. 74,600.000.00, zilipatikana kutokana na watazamaji 14,920 waliokata tiketi kushuhudia mchezo huo,  VAT(18%) tsh.11,379,661.02, CDRB (5%) tsh.3,730.000.00, FDF tsh. 5,222,000,00, TFF tsh. 2,238,000.00, Uwanja tsh. 7,804,550,85, Gharama za mchezo tsh 4,442,578.81, Bodi ya Ligi tsh. 4,162,427,12.

Chama cha soka mkoa (FA) Mbeya kimepata tsh. 1,821,061.86, FDF(TFF) tsh. 3,121,820.34, wenyeji timu ya Mbeya city wakipata tsh. 17,950,466.95 na klabu ya Yanga tsh. 12,747,438.98.

No comments:

Post a Comment