KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, February 23, 2015

TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA ALEX

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini – TFF amepeleka salamu za rambirambi kwa familia ya Alex Massawe, kufuatia kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Star) na klabu ya Simba SC, Christopher Alex kilichotokea jana mjini Dodoma.

Christopher Alex Massawe aliwahi kuichezea timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) mwanzoni mwa miaka ya 2000 kwa mafanikiko makubwa huku pia akiwa tegemeo katika klabu yake ya Simba SC.

Katika salam zake kwa familia ya Massawe, kwa niaba ya TFF, familia ya mpira wa miguu na watanzania, Rais Malinzi amewapa pole wapenzi wa mpira wa miguu nchini  katika kipindi hiki kigumu cha maombelezo.

No comments:

Post a Comment