KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 22, 2016

NGASSA, DANNY LWANGA WAMWAGA WINO FANJA FC


HATIMAYE mshambuliaji Mrisho Ngassa ameingia mkataba wa kuichezea klabu ya FC Fanja ya Oman kwa miaka miwili.

Ngassa amejiunga na Fanja wiki chache baada ya kuvunja mkataba wake wa kuichezea klabu ya Free State ya Afrika Kusini.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu za Yanga, Simba na Azam, anaungana na mshambuliaji wa Simba, Danny Lyanga, ambaye naye amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuichezea timu hiyo.

Ngassa alivunja mkataba wa miaka minne na Free State, August 25, 2016, akiwa ameitumikia mwaka mmoja pekee.

Kwa upande wa Lyanga, ambaye alikuwa hana nafasi ya kucheza Simba kutokana nafasi ya ushambuliaji kuwepo na washambuliaji kama Laudit Mavugo kutoka Burundi, Fredrick Blagnon kutoka Ivory Coast na Ibrahim Ajib, uongozi wa Simba ulimruhusu akafanye majaribio klabu ya Fanja SC.

No comments:

Post a Comment