KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 19, 2016

SERENGETI BOYS YAICHEZESHA MCHAKAMCHAKA CONGO BRAZZAVILLE




TIMU ya soka ya Taifa ya Vijana wa chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys jana ilijiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza fainali za Afrika mwakani, baada ya kuichapa Congo Brazzavile mabao 3-2.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Serengeti Boys ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.

Mshambuliaji Yohana Oscar ndiye aliyeing'arisha Serengeti Boys baada ya kuifungia mabao mawili kati ya matatu. Alifunga bao la kwanza dakika ya 38 kabla ya kuongeza la pili dakika ya 41.

Congo Brazzavile ilikianza kipindi  cha pili kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kwanza dakika ya 73 lililofungwa kwa njia ya penalti na Langa-Lesse Percy baada ya Mboungou Prestige kuchezewa rafu na beki Israel Patrick ndani ya eneo la hatari.

Dakika ya 81, 'Super Sub' Issa Abdi aliipatia Serengeti goli la tatu baada ya mabeki wa Congo kushindwa kuokoa mpira wa kona iliyopigwa na Asadi Juma kabla ya kumkuta mfungaji.

Bopoumela Chardon aliipatia Congo goli la pili dakika ya 90 baada ya wachezaji wa Serengeti kushindwa kuondoa mpira wa kona uliokua unazagaa langoni.
(PICHA KWA HISANI YA MICHUZI BLOGU)

No comments:

Post a Comment