KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 19, 2016

KILIMANJARO QUEENS YATINGA FAINALI KOMBE LA CHALENJI, YAINYUKA UGANDA 4-1

TIMU ya soka ya taifa ya wanawake ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens jana ilifuzu kucheza fainali ya michuano ya Kombe la Chalenji kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), baada ya kuibuka na ushindi wa 4-1 dhidi ya wenyeji, Uganda.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Ufundi, Njeru mjini Jinja, Kilimanjaro Queens ilijipatia mabao yote manne katika kipindi cha kwanza.

Kutokana na ushindi huo, Kilimanjaro Queens sasa itavaana na Kenya katika mechi ya fainali itakayopigwa keshokutwa.

Kenya ilitinga hatua hiyo jana baada ya kuishinda Ethiopia mabao 3-2 katika mechi nyingine ya nusu fainali.

Mabao ya Kilimanjaro Queens yalifungwa na Donosia Daniel dakika ya sita, Mwanahamisi Omari 'Gaucho' dakika ya 17, Stumai Abdallah dakika ya 31 na Asha Rashid 'Mwalala'.

Hii ni mara ya kwanza kwa CECAFA kuandaa michuano ya Chalenji kwa wanawake na iwapo Kilimanjaro Queens itatwaa taji hilo, itakuwa imeweka rekodi ya kuwa ya kwanza kulinyakua.

No comments:

Post a Comment