KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 18, 2016

SIMBA YAIKALISHA KITAKO AZAM



BAO lililofungwa na mshambuliaji Shiza Kichuya jana liliiwezesha Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Kichuya alifunga bao hilo dakika ya 67 kwa shuti kali akiwa katikati ya mabeki wawili wa Azam, baada ya kupokea pasi kutoka kwa Saidi Ndemla.

Kutokana na ushindi huo, Simba sasa imetwaa uongozi wa ligi hiyo ikiwa na pointi 13 baada ya kucheza mechi tano, ikifuatiwa na wataji wao Yanga wenye pointi 10, sawa na Azam, lakini wakiwa na mchezo mmoja mkononi.

Ushindi huo ulimpa faraja kubwa Kocha Joseph Omog wa Simba, ambaye katika msimu uliopita alikuwa kocha wa Azam kabla ya mkataba wake kuvunjwa.

No comments:

Post a Comment