KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 30, 2016

SAANYA KUZICHEZESHA SIMBA NA YANGA




SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limemteua mwamuzi Martin Saanya kuchezesha pambano la watani wa jadi, Simba na Yanga litakalochezwa kesho kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Saanya atachezesha mechi hiyo akisaidiwa na Samwel Mpenzu na Ferdinand Chacha.

Hii ni mara ya tatu kwa Saanya, mwenye beji ya Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA), kuchezesha mechi kati ya timu hizo kongwe nchini, katika miaka ya hivi karibuni.

Mara ya mwisho, Saanya alizichezesha Simba na Yanga msimu wa 2013/2014, ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Aidha, Saanya alizichezesha timu hizo msimu wa 2014/2015, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF, viingilio katika mchezo huo vinatarajiwa kuwa Sh 7,000, 10,000, 20,000 na 30,000.

Timu zote mbili zilirejea Dar es Salaam jana, Simba ikitokea mkoani Morogoro ilikokwenda kuweka kambi wakati Yanga ilikuwa imejichimbia kisiwani Pemba.

No comments:

Post a Comment