KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 1, 2016

MAAMUZI YA KAMATI YA KATIBA, SHERIA NA HADHI ZA WACHEZAJI



Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji Jumapili ya Septemba 4, 2016 inatarajiwa kutoa hukumu ya shauri la mchezaji Hassan Ramadhan Kessy anayedaiwa na Klabu ya Simba kuvunja mkataba kwa kuanza kufanya mazoezi na klabu ya Young Africans sambamba na kusajili katika timu hiyo ya Mtaa wa Jangwani, Dar es Salaam kabla ya mkataba wake kufika mwisho Juni 15, 2016.

Simba imelalamika mbele ya kamati hiyo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuwa, mchezaji Hassan Kessy alivunja taratibu hizo akiwa ndani ya mkataba wa klabu hiyo yenye mashakani yake Barabara ya Msimbazi jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati hiyo, shauri hilo lilisikilizwa na uamuzi wake utatolewa Jumapili ijayo. Hii ni baada ya kushindikana kusikilizwa kwa shauri jingine linalohusu Klabu Simba ikiilalamikia Klabu Young Africans, kuingia mkataba na mchezaji Hassan Ramadhani Kessy wakati bado ana mkataba na klabu Simba.

Shauri la Simba dhidi ya Young Africans lilishindika kusikilizwa kwa sababu Young Africans hawakutokea mbele ya kamati hiyo wakati wa kusikiliza shauri hilo, hivyo kamati itaiandikia barua Young Africans kukumbushwa kuhudhuria kwenye kesi hiyo Jumapili ijayo kabla ya kutolewa uamuzi. Kama hawakutokea tena, shauri hilo litasikilizwa upande mmoja na kutolewa uamuzi upande mmoja.

Katika mashauri mengine,

Mathias Lule v Stand United

Malalamiko ya Kocha Mathias Lule. Lule anadai mshahara, usajili na bima ya matibabu kwa Stand United. Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

Ametre Richard v Simba

Madai ya malimbikizo ya mishahara kwa Ametre Richard dhidi ya Simba. Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamekubaliana kukutana Jumatano Agosti 31, 2016 na kuleta yatokanayo TFF.

Wachezaji watatu v Mbeya City

Kamati umeamua kuwa Mbeya City ya Mbeya iwalipe wachezaji wake wa zamani, Abdallah Juma, Temi Felix na Erick Mawala madai yote ya malimbikizo ya mshahara na fedha za usajili.

Kinondoni Sports Academy (KISA) v klabu 5 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara

 (i)           KISA inadai fidia za malezi kwa Azam baada ya kumsajili mchezaji Omary Maunda, ambako Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

(ii)         KISA inadai fidia za malezi kwa Kagera Sugar baada ya kumsajili mchezaji Hussein Abdallah, ambako Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

 (iii)       KISA inadai fidia za malezi kwa Mtibwa Sugar baada ya kumsajili mchezaji Daniel Jemedari, ambako Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

 (iv)        KISA inadai fidia za malezi kwa Majimaji ya Songea baada ya kumsajili mchezaji Joseph Njovu. Shauri hili sasa litasikilizwa Jumapili ijayo ya Septemba 4, 2016 baada ya kushindikana kusikilizwa kutokana na mdaiwa Majimaji kutotokea kwenye kesi. Majimaji wameagizwa kukuhudhuria shauri hilo vinginevyo litasikilizwa upande mmoja na kutolewa uamuzi upande mmoja.

(v)          KISA inadai fidia za malezi kwa Toto African ya Mwanza baada ya kumsajili mchezaji Jafari M. Jafari, ambako Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

(vi)        KISA inadai fidia za malezi kwa JKT Ruvu ya Pwani baada ya kumsajili mchezaji Najimu Maguru, ambako Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

 SPUTANZA v Young Africans

Chama cha Wachezaji wa Mpira wa Miguu Tanzania (SPUTANZA), kilileta malalamiko dhidi ya Young Africans kuhusu madai ya usajili wa Jerry Tegete, Omega Seme na Hamisi Thabiti. Shauri hili sasa litasikilizwa Jumapili ijayo ya Septemba 4, 2016 baada ya kushindikana kusikilizwa kutokana na mdaiwa Young Africans kutotokea kwenye kesi. Young Africans wameagizwa kukuhudhuria shauri hilo vinginevyo litasikilizwa upande mmoja na kutolewa uamuzi upande mmoja.

Coastal Union v Simba SC

Coastal Union ilileta malalamiko dhidi ya Simba Sports Club kuhusu madai ya fidia ya wachezaji Ibrahim Shekwe, Hemed Hamisi na Abdi Banda. Imeamuriwa kuwa Simba iilipe mara moja Coastal Union fidia ya shilingi milioni tano.

Coastal Union v Kagera Sugar
Coastal Union ilileta malalamiko dhidi ya Kagera Sugar kuhusu madai ya fidia ya mchezaji Ibrahim Sheku. Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

Coastal Union v Mbeya City

Coastal Union ilileta malalamiko dhidi ya Mbeya City kuhusu madai ya fidia ya wachezaji Fikirini Bakari na Ayub Yahaya. Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

Coastal Union v Young Africans

Coastal Union ilileta malalamiko dhidi ya Young Africans kuhusu madai ya fidia ya mchezaji Juma Mahadhi. Shauri hili sasa litasikilizwa Jumapili ijayo ya Septemba 4, 2016 baada ya kushindikana kusikilizwa kutokana na mdaiwa Young Africans kutotokea kwenye kesi. Young Africans wameagizwa vinginevyo kukuhudhuria shauri hilo litasikilizwa upande mmoja na kutolewa uamuzi upande mmoja.

Coastal Union v JKT Ruvu

Coastal Union ilileta malalamiko dhidi ya JKT Ruvu kuhusu madai ya fidia ya mchezaji Yusuf Chuma. Shauri hili sasa litasikilizwa Jumapili ijayo ya Septemba 4, 2016 baada ya kushindikana kusikilizwa kutokana na mdaiwa JKT Ruvu kutotokea kwenye kesi. JKT Ruvu wameagizwa kukuhudhuria shauri hilo vinginevyo litasikilizwa upande mmoja na kutolewa uamuzi upande mmoja.

Bakari Shime v Mgambo JKT

Malalamiko ya Kocha Bakari Shime kudai ya mshahara dhidi ya Mgambo JKT. Kamati umeamua kuwa Mgambo JKT imlipe Shime na uongozi wa klabu hiyo umeahidi kumlipa Shime kiasi cha Sh 8,500,000 ndani ya wiki tatu kuanzia tarehe ya uamuzi huu.

Mchezaji Ally Rashid Ally v Simba

Malalamiko ya Mchezaji Ally Rashid Ally kudai kunyimwa stahiki zake na Klabu ya Simba. Shauri hili sasa litasikilizwa Jumapili ijayo ya Septemba 4, 2016 baada ya kushindikana kusikilizwa kutokana na mdai Ally Rashid Ally kutotokea kwenye kesi. Ally Rashid Ally ameagizwa kukuhudhuria shauri hilo, vinginevyo litasikilizwa upande mmoja na kutolewa uamuzi upande mmoja.

Wachezaji Omary Seseme, Said Omary na Edward Christopher v Toto African

Malalamiko ya wachezaji Wachezaji Omary Seseme, Said Omary na Edward Christopher dhidi ya Toto African kudai mishahara na fedha za usajili. Kamati umeamua kuwa Toto African iwalipe wachezaji hao na uongozi wa klabu hiyo umeahidi kumlipa ndani ya wiki mbili kuanzia tarehe ya uamuzi huu.

Wachezaji Rajab Isihaka na Said Mketo v Ndanda FC

Malalamiko ya wachezaji Rajab Isihaka na Said Mketo v Ndanda FC dhidi ya Ndanda kudai mishahara na fedha za usajili. Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

Simba SC v Mbaraka Mussa Yusufu

Simba ilileta malalamiko dhidi ya Mchezaji Mbaraka Mussa Yusufu kuhusu madai ya utoro kazini. Kamati imeridhia pande mbili kwenda kulimaliza suala hilo nje ya kamati kama ambavyo wameomba. Wamepewa wiki moja kufanya hivyo na na kuleta yatokanayo TFF.

Lipuli FC v Mbeya City

Lipuli ilileta malalamiko dhidi ya Mbeya City kumsajili mchezaji Mackyada Makolo bila kufuata utaratibu. Shauri hili sasa litasikilizwa Jumapili ijayo ya Septemba 4, 2016 baada ya kushindikana kusikilizwa kutokana na mdaiwa Mbeya City kutotokea kwenye kesi. Mbeya City wameagizwa kukuhudhuria shauri hilo vinginevyo litasikilizwa upande mmoja na kutolewa uamuzi upande mmoja.

Lipuli v Ruvu JKT

Lipuli ilileta malalamiko dhidi ya JKT Ruvu kumsajili Mchezaji Kassim Kisengo bila kufuata utaratibu ikiwa ni pamoja na kutolipa ada ya mkoa na wilaya. Pande zote mbili zilimalizana.

No comments:

Post a Comment