KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 5, 2016

STARS YAPIGWA 1-0 NA NIGERIA

HATIMAYE timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, imetupwa nje ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Afrika, baada ya kuchapwa bao 1-0 na Nigeria.

Mechi hiyo ya kundi G, iliyochezwa jana kwenye uwanja wa Uyo, Akwa Ibom, ilikuwa ya kukamilisha ratiba kwa timu zote mbili, huku Nigeria ikiwa imeshika nafasi ya pili.

Bao pekee na la ushindi la Nigeria, lilifungwa na mshambuliaji wa Manchester City, Kelechi Iheanacho, dakika ya 78.

Kipa Aisha Manula aliibuka kuwa shujaa wa Taifa Stars kutokana na kuokoa mipira mingi ya hatari iliyoelekezwa kwenye lango lake.

Kutokana na kipigo hicho, Stars imemaliza mechi za kundi hilo ikiwa mkiani, kutokana na kuambulia pointi moja, huku Misri ikiwa imeshika usukani na kufuzu kucheza fainali hizo.

No comments:

Post a Comment