KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 30, 2016

MKWASA ATANGAZA KIKOSI CHA TAIFA STARS KITAKACHOIVAA ETHIOPIA



Kocha Mkuu wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania (Taifa Stars), Charles Boniface Mkwasa ametaja majina ya nyota 24 watakaounda kikosi ambacho kitasafiri mwishoni mwa wiki ijayo kwenda Addis Ababa, Ethiopia kucheza na wenyeji wetu kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaofanyika Oktoba 8, mwaka huu.

Mkwasa maarufu kwa jina la Master amesema wachezaji aliowaita wataingia kambini Oktoba 2, 2016 kabla ya kuanza kukiandaa kuanzia Oktoba 3, 2016 ikiwa mara baada ya michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara ya mwishoni mwa wiki hii ambako Mwadui itacheza na Azam huku Mbao ikishindina na JKT Ruvu Oktoba 2, mwaka huu.

Nyota wa Stars walioitwa na Mkwasa ni:

Makipa

Deogratius Munishi – Young Africans

Said Kipao – JKT Ruvu

Aishi Manula – Azam FC

 Mabeki

Shomari Kapombe – Azam FC

Juma Abdul – Young Africans

Vicent Andrew - Young Africans

Mwinyi Haji - Young Africans

Mohamed Hussein – Simba SC

David Mwantika - Azam FC

James Josephat – Tanzania Prisons

 Viungo wa Kati

Himid Mao - Azam FC

Mohammed Ibrahim – Simba SC

Jonas Mkude – Simba SC

Muzamiru Yassin – Simba SC

Viungo wa Pembeni

Shiza Kichuya – Simba SC

Simon Msuva - Young Africans

Juma Mahadhi - Young Africans

Jamal Mnyate – Simba

Hassan Kabunda – Mwadui FC

Washambuliaji
Ibrahim Ajib – Simba SC

John Bocco - Azam FC

Mbwana Samatta - CK Genk ya Ubelgiji

Elius Maguli – Oman

Thomas Ulimwengu – TP Mazembe Congo

 Mchezo huo utakaofanyika jijini Addis Ababa, umeratibiwa kwa mujibu wa kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ambalo huwa na kalenda ya wiki ya mechi za kimataifa kwa wanachama wake – Tanzania ni miongoni mwao. Shirikisho la Mpira wa Miguu la Ethiopia (EFF), wameo

Hii ni faida kwa Tanzania kama itashinda mchezo huo kwa maana kina alama za nyongeza kama inatokea unaifunga timu mwenyeji.

Matokeo ya mchezo huo, ni sehemu malumu kupima viwango vya ubora na uwezo wa timu za taifa. Kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya 132 kati ya nchi 205 wanachama wa FIFA zilizopimwa ubora. Ethiopia yenyewe inashika nafasi ya 126.

Argentina inaongoza ikifuatiwa na Ubelgiji anakocheza Mbwana Samatta – nyota wa kimataifa wa Tanzania. Samatta anacheza klabu ya K.R.C Genk inayoshiriki Ligi Kuu ya Ubelgiji. Timu nyingine bora kimataifa ni Ujerumani, Colombia na Brazil.

Katika Bara la Afrika, Ivory Coast ambayo ni ya 34 kwa ubora duniani ndiyo inayoongoza ikifuatiwa na Algeria, Senegal, Tunisia na Ghana.

No comments:

Post a Comment