KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 29, 2016

MANJI AIPA ZAWADI YANGA SASA KUJENGA UWANJA WA KISASA.


Jiwe la Msingi la mradi wa ujenzi wa uwanja wa kisasa wa timu ya Yanga pamoja na kituo maalumu cha Kukuza vipaji vya michezo.


 Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Yanga, Mama Fatuma Karume wakati wa uzinduzi wa eneo la Uwanja lenye zaidi ya ekari 700 Geza Ulole lililopewa jina la Kijiji cha Yanga leo Jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Yanga, Mama Fatma Karume akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine wa Kamati ya utendaji ya Yanga na wawakilishi kutoka kwa wadhamini wa timu hiyo Quality Group
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MWENYEKITI wa Yanga SC, Yussuf Mehboob Manji ameipatia klabu yake eneo la zaidi ya ekari 700  lilipo Geza Ulole, Kigamboni, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Kisasa.

Akiwa amewakilishwa na wasaidizi wake  wamekabidhi eneo hilo leo mchana katika hafla fupi iliyohudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba na Maofisa wa chama na Serikali ya Kigamboni.

Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa klabu, Mama Fatma Karume akiwa ameambatana na  Mjumbe mwingine wa Bodi hiyo, Dk. Jabir Idris Katundu pamoja na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu, Samuel Lukumay, Sizya Lyimo na Kaimu katibu mkuu Baraka Deusdedit.

Eneo hilo lililopewa jina la Kijiji cha Yanga, rasmi utafanyika ujenzi wa kijiji cha michezo cha yanga ambapo patakuwa na uwanja wa kisasa wa mazoezi, uwanja wa mechi, hosteli na kituo cha kukuza vipaji kwa vijana pamoja na Hospital na shule.

No comments:

Post a Comment