KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, September 19, 2016

NGASSA AENDA KUJARIBU BAHATI YAKE ARABUNI


KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania, Mrisho Khalfan Ngassa amewasili katika nchi za Falme ya Kiarabu kwa ajili ya kucheza soka ya kulipwa.

Ngassa aliondoka nchini mwishoni mwa wiki iliyopita, kwa mwaliko wa klabu ya Fanja ya Oman, ambayo wanasoka wengi wa Tanzania wamewahi kuichezea.

"Ninakwenda Oman kufanya mazungumzo na Fanja,"alisema Ngassa wakati akijiandaa kwenda nchini humo.

Uamuzi wa Ngassa kwenda Oman umekuja wiki chache baada ya kuvunja mkataba wake na klabu ya Free State ya Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment