KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 22, 2016

SERENGETI BOYS YAPAA KWENDA KAMBINI RWANDA


TIMU ya soka ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 17, Serengeti Boys imeondoka nchini leo asubuhi kwenda Rwanda kuweka kambi ya kujiandaa kurudiana na Congo-Brazzaville.

Serengeti Boys imeondoka nchini saa tatu kamili asubuhi kwa ndege na inatarajiwa kuwasili mjini Kigali, Rwanda saa 4.30 asubuhi.

Timu hiyo inatarajiwa kurudiana na Congo-Brazzavile, wiki ijayo katika mechi ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Afrika, zinazotarajiwa kufanyika mwakani nchini Madagascar.

Katika mechi ya awali iliyochezwa wiki iliyopita, Serengeti Boys iliichapa Congo-Brazzavile mabao 3-2. Ili ifuzu kucheza fainali hizo, Serengeti Boys inahitaji sare ya aina yoyote.


No comments:

Post a Comment