KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 25, 2016

TAIFA STARS KUJIPIMA UBAVU NA ETHIOPIA


TIMU ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inatarajiwa kucheza na Ethiopia katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa, utakaopigwa Oktoba 8, mwaka huu, mjini Addis Ababa.

Mchezo huo ulio katika kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), umeombwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Ethiopia (EFF).

Iwapo Taifa Stars itashinda mechi hiyo, huenda ikapanda nafasi za juu katika ubora wa mchezo huo duniani.

Kwa sasa, Tanzania inashika nafasi ya 132 kwa ubora wa soka duniani wakati Ethiopia inashika nafasi ya 126.

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa, anatarajiwa kutangaza kikosi kitakachosafiri kwenda Ethiopia, baada ya kumalizika kwa mechi za ligi kuu zitakazochezwa Oktoba 3, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment