KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, December 2, 2013

SAMATA, ULIMWENGU WATUA NAIROBI KUONGEZA NGUVU KILI STARS



WACHEZAJI Mbwana Samata na Thomas
Ulimwengu, wamesema watahakikisha timu yao ya
Kilimanjaro Stars inacheza fainali za mwaka huu
za Kombe la Chalenji.

Ulimwengu, alitua mjina hapa juzi wakati Samata
alitua jana, tayari kuungana na Kilimanjaro Stars
katika michuano hiyo.

Samata alisema atafurahi kuona timu yake
ikicheza fainali za mwaka huu baada ya kushindwa
kufanya hivyo kwa miaka miwili mfululizo.

Alisema furaha yake ni kuona Kilimanjaro Stars
inafanya vyema katika michuano hiyo na kufika
hatua hiyo muhimu.

"Tumekosa michezo miwili ya awali katika
michuano hii, lakini mchezo wa mwisho ni lazima
tutumie nguvu zetu tukiungana na wenzetu kwa ajili
ya kuipatia ushindi timu yetu na kutinga hatua ya
robo fainali," alisema Samata.

Naye Ulimwengu alisema, hasira za kukosa ubingwa
wa michuano ya Kombe la Shirikisho wakiwa na timu
yao ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Congo, zitaishia katika michuano hii.

Ulimwengu alisema hawatapenda kuona timu yao
ikiishia katika hatua za awali za michuano hiyo na
kuongeza kuwa, wapo tayari kupambana kwa nguvu zao zote.

Samata na Ulimwengu wataungana na kikosi cha
Kilimanjaro Stars katika mchezo wa mwisho wa
kundi B itakapoivaa Burundi. Mchezo huo utafanyika keshokutwa.

1 comment:

  1. I give praise to Mr Benjamin enough for his help in securing a loan to buy our new home for our family. Benjamin was a wealth of information and he helped educate me and my family as to why a home loan was the best option for our particular situation. After conferring with Benjamin and our financial advisor everyone agreed that a home loan was the perfect solution.You can contact Mr Benjamin if you also looking for any kind of loan on Email/Whatsapp: 247officedept@gmail.com Whatsapp: +1-989-394-3740

    ReplyDelete