KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, December 2, 2013

KUZIONA TANZANITES, AFRIKA KUSINI BUKU



KIINGILIO cha chini katika mechi ya michuano ya awali ya Kombe la Dunia kwa timu za vijana wa chini ya umri wa miaka 20, kati ya Tanzania, Tanzanites na Afrika Kusini ni sh. 1,000.

Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, kiingilio hicho ni kwa viti vya rangi ya kijani, bluu na orange.

Timu hizo mbili zinatarajiwa kumenyana Desemba 7 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Pambano hilo limepangwa kuanza saa 10 jioni.

Kwa mujibu wa Wambura, viingilio vingine ni sh. 2,000 kwa VIP C, sh. 5,000 kwa VIP B wakati VIP A watalipa sh. 10,000.

Tanzanites, chini ya Kocha Rogasian Kaijage, inaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume na ule wa Taifa, Dar es Salaam, kujiandaa kwa mechi hiyo.

Wambura alisema kambi ya Tanzanites hivi sasa imehamia Msimbazi Hotel kutoka Ruvu mkoani Pwani.

Tanzanites ilivuka raundi ya kwanza baada ya kuibamiza Angola mabao 15-1. Katika mechi ya awali, ilishinda mabao 10-0 mjini Dar es Salaam kabla ya kushinda mechi ya marudiano mabao 5-1 mjini Luanda.

No comments:

Post a Comment