KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, December 4, 2013

NATAKA UBINGWA-MOURINHO


LONDON, England
JOSE Mourinho, amewataka wachezaji wa
Chelsea wawe na akili ya kutwaa
ubingwa wa ligi kuu ya England.
Kocha huyo wa Chelsea, alirudi Stamford
Bridge, Juni mwaka huu, baada ya kuiongoza
klabu hiyo kubeba ubingwa wa England mara
mbili alipotua kwa mara ya kwanza.
"Kuna maendeleo mengi yamepatikana,"
alisema kocha huyo Mreno, ambaye sasa
kikosi chake kipo nafasi ya pili nyuma ya
Arsenal.
"Kuna vitu katika kazi si rahisi na
kimojawapo ni cha kujenga presha ya kupigania
ubingwa."
"Tuna baadhi ya wachezaji waliotwaa ubingwa
kabla, lakini hawajaupata kwa muda mrefu na
ikitokea kuutwaa, wanasahau," alisema.
"Tuna wachezaji wengine waliokuwa wanacheza
katika klabu tofauti, lakini si kwa sababu ya
kutaka mataji,"aliongeza.
Alisema utamaduni wa kutaka timu iongoze
katika ligi, ikiwemo kupigana mwanzo hadi
mwisho kwa kutambua kila hatua ni muhimu
kwa sababu inaweza kuleta tofauti, inapaswa
kuwa sehemu ya maisha ya wachezaji wake.
"Ni mchakato. Si kitu unachoweza
kukifanya kwa kubonyeza. Nataka wafikiri kama
ninavyofikiri. Katika kazi yangu, napenda
kumaliza wa kwanza au nafasi ya pili na
nikishindwa nakosa raha," alisisitiza.
Chelsea jana ilicheza na Sunderland, huku
ikiwa imepitwa alama nne na vinara Arsenal.
Hata hivyo, Mourinho ametabiri timu sita
zinaweza kuwa bingwa wa England na
kuonya kuwa, Tottenham na Manchester United
hazitaendelea kufanya vibaya kwa vile zina
muda mwingi wa kurekebisha makosa.
Spurs inapitwa alama 10 na Arsenal, wakati
United imezidiwa pointi tisa na washika
bunduki hao.
"Kwa hatua hii, Spurs na Man United
zinatambua hatua inayofuata ni kupunguza
pengo la pointi kutoka 10 hadi saba (nyuma
ya vinara Arsenal) au kutoka tisa mpaka
sita ndipo zitakuwepo kwenye mbio za
ubingwa,"alisema.
"Pia nafikiri wanajua hatua inayofuata
wakipitwa kutoka pointi 10 hadi 13 au tisa
mpaka 12, mambo yatakuwa magumu,"alisisitiza kocha huyo.
 "Kwa sasa, timu kama Arsenal hazina presha
kwa sababu zikipigwa moja, hakuna
kinachowaathiri. Baadhi zinafahamu
zikianguka, hali itakuwa tete," alisema.

No comments:

Post a Comment