KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, December 4, 2013

NITAACHA UTUKUTU- BALOTELLI


MILAN, Italia
MSHAMBULIAJI mkorofi wa AC Milan, Mario
Balotelli, amesema atafanya kila awezalo
ili kuhakikisha anadhibiti hasira zake
uwanjani na hana mpango wa kuondoka San
Siro.
Nyota huyo, msimu huu amekumbwa na matukio
ya ugomvi katika mechi mbalimbali, ikiwemo
kutaka kuzichapa na Nicolas Spolli kwa
madai ya kumtolea maneno ya ubaguzi wa
rangi, AC Milan ilipocheza na  Catania.
Hata hivyo, beki huyo alisafishwa na kamati
ya nidhamu kwa madai kwamba, hakutenda kosa kinyume na
ilivyokuwa imeelezwa.
Balotelli alionyesha kuchukizwa na uamuzi
huo kwa kukebehi kupitia mtandao wa
twitter, akiandika: "Hahaha! Bahati mbaya, kuna haki
katika nchi hii."
Baada ya hapo, mshambuliaji huyo wa zamani
wa Manchester City, aliweka wazi kuwa
anataka kubadilika,na kuthibitisha kuwa
habanduki katika timu ya AC Milan.
"Kulinganisha na wakati uliopita, vitu
vingi vimebadilika, nitajaribu kubadili
tabia kabisa. Lakini nitabaki," Balotelli
aliliambia jarida la Buone Notizie.
"Nimeweka akilini mwangu mapokezi mazito
niliyopata kutoka kwa mashabiki wakati
nilipojiunga na timu hii," aliongeza.
Balotelli aliendelea kupongeza weledi wa
makocha waliomfundisha tangu alipoanza soka
hadi sasa, kwa kueleza kuwa, wamechangia
maendeleo yake licha ya kuwa na mbinu
tofauti za ufundishaji.
"Kila mmoja amekuwa na mbinu tofauti.
Roberto Mancini amekuwa kama baba, Jose
Mourinho ni mhamasishaji bora na
Massimiliano Allegri, anapenda mshikamano
katika timu," aliongeza Balotelli.

No comments:

Post a Comment