KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, December 1, 2013

EMMANUEL ASHINDA MIL 50/- ZA EBSS



MSHIRIKI Emmanuel Msuya kutoka Mwanza, juzi usiku alitawazwa kuwa mshindi wa shindano la Epiq Bongo Star Search 2013 baada ya kuwabwaga washiriki wenzake watano walioingia fainali.

Katika fainali hiyo, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Escape 1, Dar es Salaam, Emmanuel alitangazwa kuwa mshindi na jaji mkuu wa mashindano hayo, Rita Poulsen.

Washiriki watano waliotinga fainali ya shindano hilo ni Amina Chibaba,Elizabeth Mwakijambile, Emmanuel,Maina Thadei na Melisa John.

Baadaye, washiriki watatu walienguliwa na kubaki Emmanuel na Elizabeth, ambao walitinga fainali.
Kutokana na ushindi huo, Emmanuel alizawadiwa kitita cha sh. milioni 50. Alikabidhiwa fedha hizo na Rita, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Benchmark Production, inayoandaa mashindano hayo.

Emmanuel amerithi taji hilo kutoka ka Walter Chilambo, ambaye aliibuka mshindi mwaka jana.

Fainali hiyo, ambayo ilichelewa kuanza, ilipambwa kwa burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali maarufu wa Tanzania, wakiwemo Barnaba, Makomando,Young Killer, Chilambo, Shaa, Kimbunga na Snura.

No comments:

Post a Comment