KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, December 4, 2013

MATAJIRI YANGA WAMFUNGIA SAFARI OKWI



WAJUMBE wa Kamati ya Usajili ya klabu ya Yanga,
Seif Ahmed 'Magari' na Abdalah Bin Kleb wametua
mjini Nakuru kwa ajili ya kusaka wachezaji.
Seif na Bin Kleb, waliwasili Nakuru jana asubuhi na kusema
kuwa, wamekuja kuwafuatilia wachezaji watatu.
Bin Kleb, aliwataja wachezaji hao kuwa ni Emmanuel Okwi,
Daniel Ssenkuruma wa Uganda na Abdul Razak Fiston wa Burundi.
Alisema walipata taarifa za wachezaji hao kutoka
kwa mmoja wa mawakala, ambaye yupo mjini hapa
kufuatilia wachezaji.
Aliongeza kuwa, ujio wao nchini Kenya umelenga kuwaona kwa
macho wachezaji hao na pia kutathmini uwezo wao kabla ya
kuamua kuwasajili.
Bin Kleb alikiri kuwa, kwa muda mrefu Yanga imekuwa na
shauku ya kutaka kumsajili Okwi, ambaye
anamaliza mkataba na klabu yake ya sasa Februari
mwakani.
Alisema kama wataridhika na viwango vya
wachezaji hao, watakuwa tayari kumwaga mamilioni ya
fedha ili waweze kuwasajili.
"Tunachotaka ni kupata wachezaji wazuri na kila
wakala tuliyemuuliza kuhusu wachezaji hao,
aliwamwagia sifa na sasa tumekuja ili kuhakikisha
viwango vyao," alisema Bin Kleb.
Viongozi hao wa Yanga watapata nafasi ya
kumuona Abdul Razak Fiston wa Burundi wakati
timu yake itakaposhuka dimbani kuumana na
Kilimanjaro Stars katika mchezo uliochezwa jana
kwenye uwanja wa Afraha, Nakuru.
Okwi na Ssenkuruma wataonekana leo wakati timu yao ya Uganda
itakapoikabili Sudan.

No comments:

Post a Comment