KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, June 5, 2013

TBL YAZIMWAGIA VIFAA SIMBA NA YANGA



MENEJA wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe (kushoto) akiwa na viongozi wa klabu ya Yanga baada ya kuwakabidhi vifaa vya michezo kwa ajili ya michuano ya Kombe la Kagame. Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako, wa pili kulia ni Msaidizi wa Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, Geoffrey Makau akifuatiwa na Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kaziguto. (Na mpiga picha wetu).

KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL), imekabidhi vifaa vya michezo kwa klabu za Simba na Yanga kwa ajili ya michuano ya Kombe la Kagame.

Akikabidhi vifaa hivyo, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe alisema jana kuwa, vifaa hivyo vimelenga kuzisaidia klabu hizo mbili kushiriki vyema katika michuano hiyo.

Michuano ya Kombe la Kagame imepangwa kuanza Juni 18 mwaka huu, ikizishirikisha klabu bingwa kutoka nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).

"Bila ubishi Simba na Yanga ndizo klabu kubwa za mpira wa miguu Tanzania na zote zimefika katika fainali za michuano ya Kombe la Kagame kwa mara ya 19 sasa, haya ni mafanikio makubwa kwa hizi timu,"alisema Kavishe.

"Sisi kama wadhamini wakuu wa timu hizi, Kilimanjaro Premium Lager inaziunga mkono Simba na Yanga katika harakati zao za kucheza tena fainali za michuano hii ya kusisimua na ya kihistoria,"aliongeza.

Kavishe alisema Kombe la Kagame ni mashindano makubwa Afrika Mashariki na Kati na ni jukwaa bora kwa wachezaji wa Tanzania kuonyesha vipaji vyao dhidi ya wachezaji wa viwango vya juu katika ukanda huu.

Meneja huyo wa bia ya Kilimanjaro alisema mafanikio ya ushirikiano uliopo kati ya kampuni yake na klabu hizo kongwe nchini kuzishuhudia zikitoa mara kwa mara zikitoa wachezaji wengi katika timu ya Taifa, Taifa Stars.

Alizitaka klabu hizo kongwe nchini kuhakikisha zinaiwakilisha vyema Tanzania Bara katika michuano hiyo, inayodhaminiwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame.

No comments:

Post a Comment