KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, June 4, 2013

SAMATTA, ULIMWENGU WATUA MOROCCO



Taifa Stars imewasili hapa Marrakech, Morocco leo- Juni 3 mwaka huu tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itakayochezwa Jumamosi- Juni 8 mwaka huu.


Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefikia hoteli ya Pullman ambayo pia Ivory Coast ilifikia ilipokuja kucheza hapa dhidi ya Morocco. Stars imetua na wachezaji 21 huku Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu waliokuwa Maputo, Msumbiji kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho na timu yao ya TP Mazembe watawasili kesho- Juni 4 mwaka huu saa 8 mchana.

Mechi kati ya Stars na Morocco itachezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za hapa wakati nyumbani itakuwa ni saa 5 usiku.

Wakati huo huo, washambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wamejiunga na kikosi cha Taifa Stars kilichoko nchini Morocco.

Samatta na Ulimwengu waliwasili Morocco juzi mchana wakitokea Maputo, Msumbiji ambako walikwenda kuichezea timu yao ya TP Mazembe katika mechi ya michuano ya ligi ya mabingwa Afrika.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
+212610120619
Marrakech, Morocco

No comments:

Post a Comment