KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 14, 2013

SIJAACHWA, NAIFURAHIA NDOA YANGU-INI EDO


LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI mwenye mvuto wa Nigeria, Ini Edo amesema si kweli kwamba ndoa yake na mumewe, Philip Ehigwina imevunjika.

Ini aliueleza mtandao wa Nigeriafilms wiki hii kuwa, hana matatizo yoyote na mumewe na kwamba anaifurahia ndoa yake.

Baadhi ya vyombo vya habari vya Nigeria viliripoti hivi karibuni kuwa, Ini hana furaha kwa sasa kutokana na ndugu wa mume wake kushinikiza aachwe.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, ndugu wa Philip hawafurahii kuona kuwa, mcheza filamu huyo ameshindwa kumzalia mtoto ndugu yao baada ya kuolewa miaka minne iliyopita.

"Mashemeji na wakwe wa Ini Edo wamemweleza Philip amuache kama hawezi kumzalia mtoto," zilieleza taarifa hizo.

Hata hivyo, Ini amekanusha vikali taarifa hizo kwa kusema kuwa, hana matatizo na mumewe wala ndugu zake.

"Sitajali mtakachoandika kama kitabadili ukweli kwamba naifurahia ndoa yangu. Nadhani mnapaswa kuachana na uzushi huu,"alisema In.

"Tangu siku ya kwanza nilipoolewa, mmekuwa mkizusha mambo mengi ya kishetani kwangu. Sielewi ni kwa nini hamtaki kuachana na upuuzi huu. Kamwe haitatokea,"alisisitiza.

No comments:

Post a Comment