KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 14, 2013

NIMERITHI FIGA YA MAMA YANGU-OMOTOLA



LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu machachari wa Nigeria, Omotola Jalade amesema hajawahi kufanya operesheni ya aina yoyote kwa ajili ya kuupendezesha mwili wake.

Akihojiwa na gazeti la Encomium la Nigeria wiki hii, Omotola alisema amerithi umbile alilonalo kutoka kwa mama yake mzazi.

Mwanamama huyo mwenye sura na umbile lenye mvuto alisema amekuwa akifanya shughuli mbalimbali ili aweze kubaki kama alivyo.

"Hakuna siri katika mwonekano wangu, huo ndiyo ukweli ulivyo. Ukitazama picha ya mama yangu, anaonekana kama msichana. Hadi anafariki, tulizoea kumwita msichana,"alisema.

"Mama yangu alikuwa na umbile la kisichana hata alipokaribia kufikisha umri wa miaka 50. Alikuwa na umbile la kike hasa. Amenirithisha umbile hilo," aliongeza.

Omotola alisema ni kazi ngumu kulifanya umbile lake libaki kama lilivyo kutokana na mazingira ya kazi yake.

Mcheza filamu huyo aliyeolewa na rubani wa ndege na kuzaa naye watoto wanne, alisema pia kuwa hajawahi kutumia dawa za aina yoyote ili kunenepesha 'hips' zake.

"Hata mimi nimekuwa nikizisikia habari hizo, lakini hakuna kitu kama hicho. Kamwe sijawahi kutumia dawa ama kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kunenepesha hips zangu,"alisema.

"Ni suala tu la kuwa mwangalifu na makini katika mwili wangu, kazi na kila kitu,"alisisitiza mwanamama huyo, ambaye pia ni mwanamuziki.

No comments:

Post a Comment