KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, June 5, 2013

HANSPOPE AMPANDIA NDEGE KASEJA

BAADHI ya viongozi wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba wanatarajiwa kuondoka nchini kati ya leo na kesho kwenda Morocco ili kumalizana na kipa Juma Kaseja.

Kaseja yuko nchini Morocco akiwa na kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars kinachotarajiwa kurudiana na timu ya taifa ya nchi hiyo keshokutwa katika mechi ya michuano ya awali ya Kombe la Dunia.

Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hanspope anatarajiwa kwenda Morocco akitokea Libya, ambako alikwenda kukamilisha usajili wa mchezaji wa kimataifa wa Uganda, Moses Oloya.

Habari kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa, Hanspope alimalizana na mchezaji huyo wa Uganda mara baada ya timu ya taifa ya nchi hiyo kuchapwa mabao 3-0 na Libya mjini Tripoli.

Kwa mujibu wa habari hizo, lengo la vigogo hao wa Simba kwenda Morocco ni kumbembeleza Kaseja ili aongeze mkataba mpya wa kuichezea klabu hiyo.

Mkataba wa Kaseja kuichezea Simba ulimalizika mwishoni mwa msimu huu na kuna habari kuwa, amekuwa akiwaniwa na klabu ya Azam.

Awali, kamati ya usajili ya Simba ilikuwa imegawanyika kuhusu usajili wa mchezaji huyo, lakini baadaye imeona kuna umuhimu wa kumuongezea mkataba.

No comments:

Post a Comment