KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 14, 2013

WASOMAJI WA LIWAZOZITO WALIVYOMLILIA MANGWEA


Much respect kwa makala yako. Media zimekuwa na unafiki baada ya msanii kufariki dunia. 0759928344

Uko sawa kaka, yaani wanakera sana.0774401918.

Ni ukweli usiopingika kipindi cha uhai wa Mangweha nyimbo zake hazikusikika redioni wala kwenye televisheni, ila kila siku ya kifo kuna redio zilishinda zinapiga nyimbo zake. Enzi za uhai wake hatukuweza kusikia wimbo wa Mangweha hata mara moja kwa mwaka. Ni ukweli kuwa wasanii wa Tanzania wananyonywa sana na yakitokea mambo kama haya wanaanza kumsifia ujinga, alikuwa mtu wa watu, alikuwa mpole, jamani tumuogope Mungu, uwezo uliopewa na Mungu kisiwe kigezo cha kuwakandamiza wenzako, chonde chonde. 0752752132 Katoro-Geita.

Ipo siku moja watajuta kwa dhambi waliyomfanyia mangweha. 0774629813

Pole na kazi, nakupongeza kwa kuandika makala ya kifo cha mangweha, tunamlilia mangweha baada ya kufa. Safi sana, unajua kazi.Bukoba. 0754648041.

Ebwana kaka Baligeya, mi naitwa Seif Omary, nipo UDOM mwaka wa kwanza Kiswahili Fasihi, yaani uliyoandika ni ukweli kabisa, lakini ni vyema yasiishie hapa, uendelee kuandika makala kama hizi ili kuwaamsha wasanii mazuzu wasiojitambua.0769867781.

Mambo vipi mkubwa, nimelisoma gazeti la Burudani na kusoma makala yako inayohusu kifo cha mangweha. Kiukweli hata mimi ilikuwa inaniboa kila stesheni kupiga nyimbo zake tena na kutoa wasifu wake. Kama kweli wapo karibu naye, mbona hawakutangaza anakwenda Afrika Kusini wakati alipokuwa hai. Hizi stesheni za redio ni za kinafiki. 0719522328.

Ni kweli ndugu vyombo vya habari baadhi ni wanafiki. Mungu huwa analipa hapa hapa duniani, leo kwa huyu, kesho kwao.0764157865

Bwana Stephen Baligeya, umeongea yaliyokuwa moyoni mwangu (Tunamlilia mangweha baada ya kufa). Ni kweli kabisa kwamba vipo vyombo vya habari vinavyoua masoko ya wasanii na kuwafanya waishi kwa shida. Vyombo hivyo tunavijua mpaka majina. By Mzaile Bokilo, nipo Misungiwi-Mwanza 0757283585.

Kaka nakupa pongezi kwa kutowaonea haya waliomnyonya Mangweha mpaka kabaki mifupa mitupu. Matatizo yote wamesababisha wao. Hili ni fundisho kwa wasanii wa bongo, ningependa wamuunge mkono P Funk.

Tatizo la wasanii wa Tanzania hawana kauli moja.0752805090.

Habari kaka, naitwa Paskacaly Mbasha. Kiukweli mi mwenyewe sikuamini kile kilichosemwa na vyombo vya habari kwamba Mangweha ametoweka duniani. Lakini nimekuja kuamini katika kuaga mwili wake.

Machozi yalinitoka bila mwenyewe kujielewa. Inauma sana brother. Kiukweli umimi ndio unaangamiza au unashusha maendeleo ya wasanii wetu. Kumpaisha mwenzako sidhani kama wewe unaweza ukabaki chini, tumekuwa mbele na kujionyesha tunawajali pale wanapopatwa na mauti, tunawasahau pale wanapokuwa na matatizo. Kama kukusanya michango na kuweka majukwaa inawezekana, inashindikana vipi kufanya hivyo wakiwa hai? Naungana na wewe kuwa ni wanafiki na wazandiki, kuweka majukwaa na kupigwa nyimbo zake utadhani wanasherehekea badala ya kuomboleza. Big up brother.0768839171.

Ebwana kaka unatisha. Nimependa makala yako kuhusu kifo cha Mangweha. Umesema mambo ambayo hata mimi yamenikera kabisa. Big up. Kutoka Mwanza.0769096013

Kaka makala yako imenigusa, lakini ungefanya kudokeza kidogo hizo stesheni za radio ili tuwajue waliojifanya wanampenda Mangweha wakati wa mauti kuliko kutuacha na mafumbo.0766915346.

Naomba hizo stesheni zianikwe ili nyingine ziogope. Haiwezekani msanii afe ndio apate umaarufu. Wengine leo ndio wanamjua Mangweha. Naitwa Joseph Sanga kutoka Igunga Tabora.0768603090.

Nakupongeza sana kwa kulijua hili na kupata ujasiri wa kulizungumzia. Itakuwa fundisho kwa vyombo vya habari.0714136226.

Kaka makala hii ya Mangweha umesema ukweli na mimi sina zaidi ya kuunga mkono juu ya jambo hili. Uko sahihi na kuna wasanii wangelitambua hili mpaka leo hii Mangweha angekua hai.0659380040.

Mbona kwenye makala yako unakandamiza chombo kimoja tu cha habari? Kama kweli wewe umekereka, ungetaja media zote sio kuponda sehemu moja tu. Hata sisi wananchi tuna makosa kwa sababu hatutoi support kwa wasanii wetu, hatupaswi kulaumiana.0653936885.

Salute mkuu Baligeya! Nimesoma makala yako, umewachana ndani na nje hawa wanafiki wanaochukulia msiba wa Mangweha kujipatia sifa za kijinga, hasa hawa wanaojiita masupa staa. Naamini walikuwa hata hawajui safari yake ya Afrika Kusini.0764920545.

Umeandika ambacho mimi pia kimeniuma sana, lakini nilikuwa sina pa kusemea. Nafikiri umewakilisha Watanzania wengi walio werevu wa fikra! Najua itakujengea maadui wengi sana kwa ukurasa huo mmoja tu ambao umeelimisha watu wengi kwa wakati mmoja. ‘Only God knows’. 0752809939.

Ukweli kabisa Mangweha alishasahaulika kwenye gemu la muziki wa kizazi kipya. Sasa kafariki amevuma, amekuwa gumzo kila kona bila faida kwake.0652316053.

Hilo hata mimi nakubaliana nalo maana leo hii Mangweha angekuwa tajiri sana, lakini maskini ya Mungu wako wanaokula vizuri , kulala vizuri kupitia mgongo wake. Wasanii wanatakaiwa wafikirie sana juu ya hili, angalau wamuone hata yule Mama Mangweha. I love you bro RIP Mangweha. Husna wa Arusha.0767189858.

Nashangaa hawana chembe ya aibu. Msanii akirekodi kwa P Funk inakuwa shida. Tazama Jay Mo na Mangweha wamezimwa na ndo wamebadili ngoma kali. Kwa kifo hiki, wabadilike. Kutoka Kiteto.0782501774.

Ni vibaya kumfanyia uovu mtu halafu akifa uwe mstari wa mblele kumzika. Nafsi zao zinawasuta. Watanzania tunasikia hayo na ipo siku yatafika mwisho. Haipendekezi wewe mwenyewe uwe stari wa mbele bila kushirikisha wenzio mwanzo hadi mwisho wakati nyimbo za marehemu Mangweha zinapigwa na stesheni zote na kusikika na rika lolote. Zaidi msanii ni nguzo imara kufikisha ujumbe kwa vijana wote kiurahisi. Tumepoteza askari mshauri. Wasanii wawe na chama chao chenye kuratibu mambo yao.089575789.

Nimemaliza kusoma makala yako kuhusu kifo cha msanii Mangweha bila shaka ujumbe utakuwa umewafikia wahusika. Asante.0717796037.

Hawa makupe ni wajinga na watu wasiofaa hata kidogo. Sielewi kwa nini wakati alipokuwa hai, hawakutaka kupiga nyimbo zake. Walimchukulia Mangweha kama mtu asiyekuwa na maana. Leo hii amekufa, wanampamba sifa kibao na kujiweka kimbelembele. Kinachokera zaidi ni kwamba wanajisifu kwamba walimsaidia alipokuwa hai. Nawachukia sana watu hawa kwa unyonyaji wao kwa wasanii. 0713941101.

Habari ya asubuhi! Nimesoma makala yako ya 'Tunamlilia Mangweha baada ya kufa! Kwa kweli upo sahihi kabisa. Nakutakia mafanikio mema katika kazi yako ya uandishi wa habari. Naitwa Bahati Kiula mkazi wa Mikocheni B, Dar es Salaam.

Yaani makala yako imenigusa na kuniumiza moyo wangu sana na hapa nilipo mazungumzo ni hayo ya Mangweha na hizo redio. Kama ulinikataa nilipokuwa hai, hata nikifa usinikubali. 0717353370

Habari brother. Mimi ni mtanzania, naishi Kilimanjaro. Nimeguswa sana na mada yako kuhusu kifo cha Mangweha. Ushauri wangu naomba hivyo vyombo vya habari, ambavyo vina tabia hiyo, muwaweke hadharani watanzania wote watambue kwani huo ni unyama uliokithiri. Inauma sana kuona vijana wetu wanajituma sana, lakini kuna watu wanawamaliza. Iwapo itadhihirika ni kweli, sheria ichukue mkondo wake wafungwe. 0753616171.

Mambo vipi kaka? Uko poa? Mimi mzima wa afya. Nakupongeza sana kaka kwa kuitoa nakala yako kwenye gazeti la Burudani. Baligeya wewe ni mwandishi wa habari, ambaye una mtazamo wa mbali sana. Hawa watu wanaojiona bora katika mambo ya habari ni wabaya sana.

Wanawaua wasanii na muziki huu kwa jumla. Leo Albert Mangweha anaonekana ana thamani wakati tayari amekuwa marehemu. Kipindi alipokuwa hai walikuwa hawamthamini na nyinbo zake hawazichezi. Mungu atamlipia Mangweha kwa unafiki waliomtendea. Endelea hivyo kaka, kusema maneno yaliyo ya kweli na Mungu atakuongoza na kubariki kazi za mikono yako—RIP ALBERT MANGWEHA-ailaze roho yako mahali pema peponi amina. Mangole.0714057304.

Safi sana kaka Stephen Baligeya kwa makala hii ya Mangweha. Tatizo letu watanzania linabaki palepale, unafiki. Hata wewe unawajua waziwazi wanaowaua wasanii na watakaoua wengine pia kwa kuwachanganya kiakili, lakini kama hautawataja moja kwa moja kuwa ndio chanzo cha yote haya, sote tutabaki pale pale na wao wataendelea kufanya yale yale. Atakufa mwingine na wengine mpaka Tanzania tutakapoamua kuambiana ukweli bila kupepesa.0717340184.

No comments:

Post a Comment