KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, June 4, 2013

MWILI WA MANGWEA WATUA DAR


Mamia ya watu jana walijitokeza kuupokea mwili wa aliyekuwa msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Albert Mangwea.

Vilio na simanzi vilitawala kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam wakati mwili wa msanii huyo ulipowasili saa 8.00 mchana kwa ndege ya Shirika la Ndege la Afrika Kusini.

Mwili wa marehemu Mangwea unatarajiwa kuagwa leo kuanzia saa 2.00 asubuhi kwenye viwanja vha Leaders vilivyopo Kinondoni, Dar es Salaam kabla ya kusafirishwa kwenda Morogoro kwa ajili ya mazishi.

No comments:

Post a Comment