KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, June 14, 2016

SERENGETI BOYS WAINGIA KAMBINI LEO


Timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kinaingia kambini leo Juni 14, 2016 kujiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya vijana wenzao wa Shelisheli utakaofanyika Juni 26, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Mchezo wa marudiano kati ya Serengeti Boys na Shelisheli utachezwa Julai 2, 2016 huko Shelisheli.

Makipa:
Kelvin Deogratius Kayego,

Ramadhani Awm Kambwili na
Samwel Edward Brazio.

Mebeki wa Pembeni:

    Kibwana Ally Shomari,
    Israel Patrick Mwenda,
    Anton Shilole Makunga na
    Nickson Clement Kibabage.

Mabeki wa Kati:

    Dickson Nickson Job
    Ally Hussein Msengi na
    Issa Abdi Makamba

Viungo wa Kuzuia:

    Kelvin Nashon Naftal
    Ally Hamis Ng’anzi na
    Shaban Zuberi Ada

Mawinga:

    Mustapha Yusuph Mwendo
    Yassin Muhidini Mohammed
    Syprian Benedictor Mtesigwa na
    Gadafi Ramadhan Said

Viungo wa kushambulia:
    Asad Ali Juma
    Mohammed Abdallah Rashid na
    Muhsin Malima Makame

Washambuliaji:

    Ibrahim Abdallah Ali
    Enrick Vitaris Nkosi
    Rashid Mohammed Chambo na
    Yohana Oscar Mkomola

Katika kuajindaa na mchezo huo, Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako walishiriki mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na FIFA (AIFF International Youth Tournament 2016) kabla ya kurudi na rekodi ya kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa nchi za Afrika Mashariki.

Kadhalika Serengeti Boys ilicheza mfululizo michezo saba ya kimataifa bila kufungwa dhidi ya Misri (2), India, Korea Kusini, Malaysia na Marekani (USA). Kabla ya hapo timu hiyo ilicheza michezo kadhaa ya ndani na timu za chini ya umri wa miaka 20 bila kupoteza hata mchezo mmoja.

Katika mashindano ya AIFF, timu hiyo pekee kutoka Afrika na ambayo ilikua kipenzi cha mashabiki katika jiji la Goha ilicheza na timu ambazo ziko juu katika hatua za juu katika mtoano wa kuwania kushiriki Kombe la Dunia kupitia mabara yao yaani CONCACAF (USA) na AFC (India, Korea na Malaysia).

No comments:

Post a Comment