KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, June 27, 2016

SERENGETI BOYS YAIPIGA SHELISHELI MABAO 3-0


TIMU ya soka ya Taifa ya vijana wa chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys jana ilijiweka kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kucheza fainali za Afrika baada ya kuichapa Shelisheli mabao 3-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Serengeti Boys ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.

Kwa ushindi huo, Serengeti Boys sasa inahitaji sare ya aina yoyote katika mchezo wa marudiano utakaochezwa wiki mbili zijazo nchini Shelisheli.


No comments:

Post a Comment