KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 30, 2016

KOCHA TWIGA STARS ATANGAZA KIKOSI KITAKACHOMENYANA NA RWANDA


Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Mpira wa Miguu ya Wanawake Tanzania, Nasra Juma ametangaza majina ya wachezaji 23 watakaounda kikosi cha Twiga Stars.

Kikosi hicho kinatarajiwa kwenda Kigali, Rwanda Julai 15, 2016 kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Rwanda ikiwa ni mwaliko maalumu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Rwanda (Ferwafa).

Wakati Ferwafa likiingiza mchezo huo wa Julai 17, 2016 kwenye orodha ya michezo inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira na Miguu la Kimataifa (Fifa), lakini Mheshimiwa Rais wa Rwanda Paul Kagame kuwa sehemu ya burudani ya burudani mbele ya wageni wake ambao ni wakuu mbalimbali wanaounda Umoja wa Nchi za Afrika (AU) ambao watakuwa na mkutano wao nchini Rwanda.

Mbali ya soka kama burudani, pia Rais Kagame atatumia mchezo huo kama hamasa kwa wakuu wa nchi ili kutoa kipaumbele kwenye soka la wanawake ambako kwa sasa ni ajira ambayo inakwenda sambamba na kuitikia wito wa kupambana na changamoto za malengo ya millennia (MCC) ambayo pia yanataka wanawake wapate nafasi.

Makipa:

Fatma Omary
Belina Julius
Najiat Abbas

Walinzi:
Stumai Abdallah

Fatma Issa
Anastazia Antony
Happuness Henziron
 Maimuna Khamis



Viungo:
Donisia Daniel

Amina Ali
Amina Ramadhani
 Fatuma Bashiri
 Wema Richard
  Fadhila Hamadi
  Mwajuma Abdallah
  Anna Hebron
  Sophia Mwasikili

Washambuaji:
Tumaini Michael
 Johari Shaaban
 Fatma Idd
 Shelder Bonifdace Mafuru
 Asha Saada Rashid
 Mwanakhamisi Omar

No comments:

Post a Comment