KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, September 26, 2015

TFF YATUMA RAMBIRAMBI BAKWATA


Rais wa Shrikisho la Mpira wa Migu nchini (TFF), Jamal Malinzi ametuma salam za rambirambi kwa Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry kufuatia vifo vya mahujaji zaidi ya 700 vilivyotokea Maka wakati wa kuhiji.

Katika salam zake kwenda kwa mufti mkuu, Malinzi amewapa pole waislam wote duniani kufuatia vifo vya mahujaji hao zaidi ya 700 vilivyotokea juzi na majeruhi zaidi ya 400 wakati wa ibada ya hija.

Malinzi amesema kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini TFF inawapa pole wafiwa wote, ndugu jamaa na marafiki na kuwatakia majeruhi afya njema na kusema ipo pamoja nao katika kipindi hichi kigumu cha maombelezo.

No comments:

Post a Comment