KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, September 16, 2015

AZAM YAENDELEA KUCHANUA



AZAM FC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada kuwalaza mabao 2-0 wenyeji Stand United Uwanja wa Kambarage, Shinyanga jioni ya leo.
Shukrani kwao, wafungaji wa mabao hayo, mshambuliaji wa Kenya, Alan Watende Wanga na kiungo mzalendo Frank Rymond Domayo.
Huo ushindi wa pili mfululizo kwa Azam FC ya kocha Muingereza Stewart Hall, baada ya awali kuichapa Prisons ya Mbeya 2-1 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Katika mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Yanga SC imeialza 3-0 Prisons Dar es Salaam, Simba SC imeifunga 2-0 Mgambo JKT Tanga, Majimaji FC imeifunga 1-0 Kagera Sugar Songea, Mbeya City imeichapa 3-0 JKT Ruvu Mbeya, Toto Africans imefungwa 2-1 na Mtibwa Sugar Mwanza, Ndanda FC imeialza 1-0 Coastal Union Mtwara na Mwadui FC imeshinda 2-0 dhidi ya African Sports.

MATOKEO MECHI ZA LIGI KUU TZ BARA LEO
Yanga SC 3-0 Prisons
Mgambo JKT 0-2 Simba SC
Majimaji FC 1-0 Kagera Sugar
Mbeya City 3-0 JKT Ruvu
Stand United 0-2 Azam FC
Toto Africans 1-2 Mtibwa Sugar
Ndanda FC 1-0 Coastal Union
Mwadui FC 2-0 African Sports
IMETOLEWA KUTOKA BLOGU YA BINZUBEIRY

No comments:

Post a Comment