KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, September 30, 2015

KIKOSI CHA U-15 CHAENDA TANGA KUJIPIMA NGUVU



Kikosi cha Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U15) kinatarajiwa kusafiri kesho Jumatano kuelekea jijini Tanga kwa ajili ya mchezo wa kirafiki na kombani ya U15 ya jijini humo.

U15 ambayo iliingia kambini siku ya Ijumaa katika hosteli za TFF zilizopo Karume imekua ikifanya mazoezi asubuhi na jioni katika uwanja wa Karume kujiandaa na michezo hiyo ya kirafiki itakayofanyika siku ya Alhamis na Ijumaa.

Kocha Mkuu wa timu hiyo Sebastian Nkoma anatarajiwa kutumia michezo hiyo ya kirafiki jijni Tanga kuona maendeleo ya vijana wake na kupata kung’amua vipaji vingine atakavyoviona katika mchezo kwa ajili ya kuboresha kikosi chake.

Program hiyo ya vijana ilianza mwezi Juni mwaka huu ambapo kila mwisho wa mwezi, wachezaji hao hukutana jijini Dar es salaam kwa ajili ya kambi kabla ya kusafiri mikoani kucheza michezo ya kirafiki.

Mpaka sasa kikosi hicho cha vijana wenye umri chini ya miaka 15 kimecheza michezo ya kirafiki na kushinda michezo yote katika mikoa ya Mbeya, Zanzibar, na kutoka sare na kombaini ya Morogoro.

Wachezaji waliopo kambini wanaotarajiwa kusafiri kesho ni Josephat Mbokiwe, Anthony Shilole, Kelvin Deogratius, Maziku Amede, Hamis Juma, David Julius, Kibwana Ally, Mohamed Ally, Ibrahim Ramadhan, Frank George, Maulid Salum.

Wengine ni Faraji John, Athuman Maulid, Mwinjuma Abdallah, Alex Peter, Ibrahim Abdallah, Rashid Kilongora, Casto Issa, Ally Hussein, Jama Idd, Asad Ally na Issa Abdi.

No comments:

Post a Comment