KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 13, 2015

SIMBA YAANZA VYEMA LIGI KUU, YAICHAPA AFRICAN SPORTS 1-0


SIMBA SC imeanza vyema Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji African Sports Uwanja wa Mkwakwani, Tanga jioni ya leo.
Shukrani kwake mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Friday Kiiza ‘Diego’ aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 56, akimalizia kwa kichwa krosi maridadi ya Nahodha Mussa Hassan Mgosi.
Simba SC ilicheza vizuri tangu mwanzo wa mchezo na kukaribia lango la wapinzani mara kadhaa, lakini uhodari wa kipa wa zamani wa Yanga SC, Yussuf Abdul uliwanyima mabao zaidi Wekundu hao wa Msimbazi.
Pamoja na kwamba imepanda msimu huu, African Sports maarufu kama Wana Kimanumanu walionyesha upinzani kwa Simba SC
Mshambuliaji Boniphace Maganga aliyesajiliwa msimu huu kutoka Marsh Academy ya Mwanza, alikosa bao la wazi baada ya kuunganishia juu ya lango krosi nzuri ya Simon Sserunkuma dakika ya 89.
Hussein Amir aliinyima Sports bao la kusawazisha dakika ya 90, baada ya kuunganishia juu ya lango krosi nzuri ya Ayoub Masoud.
Katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu leo, Azam FC imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Prisons ya Mbeya Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Shukrani kwake Farid Mussa aliyefunga bao la ushindi dakika ya 86 baada ya Jeremiah kuisawazishia Prisons dakika ya 60, kufuatia
Kipre Herman Tchetche kuanza kuifungia Azam FC dakika ya 42.
Kikosi cha African Sports kilikuwa; Yusuph Yusuph, Ayubu Masoud, Mwaita Gereza, Juma Shemvuni, Rahm Abdallah, Novat Lufungo, Jemes Mendi/Ally Ramadhani dk83, Husein Amiri, Hasani Matemema, Omary Issa, Pera Mavuo/Bakari Masoud dk53.
Simba SC; Peter Manyika, Mohamed Husei ‘Shabalala’ Hassan Kessy, Jjuko, Majabvi, Awadh Juma, Said Ndemla, Mwinyi Kazimoto/Simon Sserunkuma dk89, Mussa Hassan ‘Mgosi’,Hamisi Kiiza/Boniphace Maganga dk75 na Peter Mwalinyanzi.
IMETOLEWA BLOGU YA BINZUBEIRY

No comments:

Post a Comment