KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, September 2, 2015

NIGERIA KUTUA DAR KESHO


Timu ya Taifa ya Nigeria (Super Eagles) inatarajiwa kuwasili kesho AlhamisI saa nne usiku kwenye uwanja wa JK Nyerere jijini Dar es salaam kwa usafiri wa ndege binafsi tayari kwa mchezo dhidi ya Tanzania siku ya jumamosi uwanja wa Taifa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Nigeria (NFF), kupitia kwa Toyin Ibitoye msafara huo unatarajiwa kuwa na wachezaji 23 pamoja na viongozi wa benchi la ufundi linaloongozwa na kocha mkuu Sunday Oliseh pamoja na viongozi wengine waandamizi wa shirikisho hilo.

Nigeria inatarajiwa kufanya mazoezi siku ya ijumaa saa 10 jioni katika uwanja wa Taifa, ikiwa ni mazoezi mepesi ya kuelekea kwenye mchezo huo.

KOZI YA UKOCHA LESENI B YAFUTWA Z'BAR
 Kozi ya makocha wa CAF ya Leseni B iliyokua ifanyike kwa muda wa wiki tatu mwezi Septemba mwaka huu kisiwani Zanzibar sasa imefutwa kufuatia kupeleka mpira mahakamani.

Sasa kozi hiyo itafanyika tena pindi kesi ya mpira itakapoondelewa mahakamani. Kumekua na hali ya kutokuelewana kwa uongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu kisiwani Zanzibar (ZFA) hali iliyopelekea uongozi wa ZFA kupelekwa mahakamani.

Kwa mujibu wa kanuni za FIFA, masuala ya mpira wa miguu hayapaswi kupelekwa mahakamani



No comments:

Post a Comment