KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 13, 2015

DK. FEENELLA KUZINDUA MICHUANO YA AIRTEL RISING STAR



 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dr. Fenella Mkangara leo Jumapili, Septemba 13, 2015 saa 8 kamili mchana anatarajiwa kuzindua rasmi fainali za michuano ya Airtel Rising Star katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Jumla ya timu sita zinatarajiwa kushiriki michuano hiyo ambayo imekua ikifanyika kila mwaka nchini kwa udhamini wa kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, ambapo vijana wenye vipaji huchaguliwa na kupata nafasi ya kujiunga na vituo vya michezo (Academy) za Dakara – Senegal na Doha – Qutar zinazomilikiwa na kampuni hiyo.

Katika uzinduzi huo wa leo, timu za mkoa wa Ilala, Kinondoni, Mbeya, Morogoro, Mwanza na Temeke zinatarajiwa kupambana kusaka mshindi kwa fainali hizo za kitaifa.

Shirikisho la Mpira Miguu nchini (TFF), limetuma salamu za rambirambi kwa familia za Lubawa,  kufutia kifo cha mwamuzi mstaafu na kamishina wa TFF Saleh Lubawa kilichotokea jana jioni.

Katika salam zake kwenda kwa familia ya marehemu, TFF imesema inawapa pole wafiwa, ndugu jamaa na marafiki na kwa niaba ya familia ya mpira miguu nchini wapo pamoja na familia katika kipindi hichi cha maombolezo.

Mazishi ya marehemu Saleh Lubawa yanatarajiwa kufanyika leo jioni nyumbani kwake eneo la Kongowe – Kibaha.

No comments:

Post a Comment