KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 6, 2015

TAIFA STARS YATOKA SULUHU NA NIGERIA




Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeshindwa kuutumia vyema uwanja wake wa nyumbani baada ya kulazimishwa suluhu ya bila kufungana na timu ya Taifa ya Nigeria ‘Super Eagles’.
Stars itabidi ijilaumu kwa kushindwa kutoka na ushindi katika mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la Taifa kwani ilitengeneza nafasi nyingi za kufunga ukilinganisha na wapinzani wao.
Thomas Ulimwengu, Mrisho Ngassa na Mbwana Samatta walipoteza nafasi za wazi za kuweka mpira wavuni huku kipa wa Nigeria akiibuka nyota wa mchezo kutokana na kuzuia mashambulizi mengi yaliyokuwa yakifanywa na wachezaji wa Stars.
Shukrani za pekee zimuendee Charles Boniface Mkwassa na benchi lake la ufundi kutokana na kuboresha kiwango cha Stars kwani licha ya kutopata ushindi leo, timu imeonekana ikicheza kwa kuelewana.
Nigeria imefikisha pointi nne kutoka michezo miwili baada ya matokeo ya leo, iko kileleni wakati Taifa Stars ina pointi moja.
Misri itakwaana na Chadi kesho katika mchezo mwingine wa kundi la Stars

No comments:

Post a Comment