KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 13, 2015

MABAO 10 YATINGA MECHI ZA AWALI LIGI KUU, AZAM YAILAZA PRISONS 2-1


MABAO 10 tu yametinga nyavuni katika mechi  saba za ufunguzi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo, huku kipa mpya wa Mbeya City, Juma Kaseja akianza vibaya Uwanja wa Sokoine.
Kaseja amefungwa bao moja  na timu yake mpya ikilala 1-0 nyumbani mbele ya Kagera Sugar kutoka Bukoba na hakuna timu iliyoshinda kwa wastani wa zaidi ya bao 1-0 dhidi ya wapinzani wake.
Timu zote zote zimeshinda 1-0 na 2-1 baada ya mechi zote saba leo.
Kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga Simba SC imewafunga bao 1-0 wakati Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, Ndanda FC imelazimishwa sare ya 1-1 na Mgambo Shooting ya Tanga.
Uwanja wa Majimaji, Songea  wenyeji Majimaji FC wameshinda 1-0 dhidi ya JKT Ruvu, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Azam FC imeshinda 2-1 dhidi ya Prisons wakati Toto Africans imeshinda 1-0 dhidi ya Mwadui FC.
Timu zilizoanza kwa ‘mikosi’ zaidi Ligi ya msimu huu ni Stand United iliyofungwa 1-0 na Mtibwa Sugar Uwanja wa Kambarage, Shinyanga na Mbeya City iliyofungwa 1-0 na Kagera Sugar Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania itaendelea kesho wakati mabingwa watetezi, Yanga SC watakapomenyana na Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
IMETOLEWA KUTOKA BLOGU YA BINZUBEIRY

No comments:

Post a Comment