KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, September 23, 2015

STAR TIMES KUDHAMINI LIGI YA FDL



Kampuni ya StarTimes Media ya jijini Dar es salaam leo imeingia mkataba wa udhamini na TFF kudhamini Ligi Daraja la Kwanza nchini (FDL) inayoshirikisha timu 24 kutoka katika mikoa 16 ya Tanzania bara.

Akiongea na waandishi wa habari wakai uwekaji sahihi mkataba huo, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi ameshukuru kituo cha Star Times kwa kuamua kuwekeza katika mpira wa miguu na hasa kwenye chimbuko la vipaji na wachezaji wengie nchini.

Malinzi amesema udhamini huo wa shilingi milioni 900 kwa kipindi cha miaka mitatu, unatarajiwa kuongezeka wiki ijayo baada ya kuingia mkataba na mdhamini mwingine wa kurusha matangazo ya ligi hiyo kwa shilingi milioni 450 na kufikia jumla ya udhamini wa shilingi bilioni 1.3.

Aidha Malinzi amesema TFF inaendelea na mipango ya kuhakikisha inavisaidia vilabu vya madaraja ya chini, timu za wanawake na vijana kuona vinapata udhamini na kuweza kushirki vyema michuano mbalimbali.

Naye Mkurugenzi wa StarTimes Media nchini, Lanfang Liao amepongeza ushirikiano mpya ulioanzishwa kati ya kampuni yake na TFF na kuahidi kudumisha ushirkiano huo kwa faida ya maendeleo ya mpira wa Tanzania.

Mwenyekiti wa timu ya Kinondoni Municipal Council (MKC), John Njunde akiongea kwa niaba ya vilabu vya ligi daraja la kwanza, amesema anaishukru TFF kwa kuweza kuvitafutia udhamini vilabu na sasa wataweza kushiriki vizuri ligi hiyo inayotoa timu tatu zitakazopanda ligi kuu msimu ujao.

No comments:

Post a Comment