KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, September 13, 2015

DRFA YAZINDUA KOZI YA UKOCHA LESENI C




Chama cha soka mkoa wa Dar es salaam,DRFA kwa kushirikiana na shirikisho la soka nchini TFF,leo imezindua rasmi kozi ya ukocha wa leseni C’ inayotambuliwa na shirikisho la kandanda barani afrika CAF.

Kozi hiyo ya wiki mbili inaendeshwa na mkufunzi, Salum Madadi ambaye ni mkurugenzi wa ufundi wa Tff,ikiwa na jumla ya washiriki 31 wengi wao wakiwemo makocha wa vilabu vya ligi daraja la pili,daraja la kwanza na ligi kuu.

Miongoni mwa washiriki hao ni pamoja na kocha msaidizi wa Simba,Suleiman Matola,katibu mkuu wa zamani wa Simba Muhina Kaduguda,kocha wa Ruvu shooting Tom Olaba,kocha wa makipa wa Yanga Juma Pondamali,nyota wa zamani wa Taifa Stars,Ally Mayai na Peter Tino.

Mgeni rasmi katika ufunguzi wa kozi hiyo ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya Tff,Msafiri Mgoy,ambaye amewapongeza washiriki kwa uamuzi wao wa kutaka kujiongezea maarifa ya ufundishaji wa soka ,kwa kuwa Tanzania inakabiliwa na upungufu mkubwa wa makocha ikilinganishwa na mataifa mengine ya Afrika ambayo yamepiga hatua kisoka.

Aidha amesema Tff imeweka mpango maalum wa kutunza kumbukumbu za makocha hao na wengine watakaopatikana,pamoja na kufuatilia kazi zao kwenye vilabu mbalimbali watakavyofundisha ili iwe rahisi kuwatengenezea mazingira mazuri ya kufanya kazi zao.

Naye mwenyekiti wa DRFA,Almasi Kasongo wakati akimkaribisha mgeni rasmi,amesema chama chake kinataraji pia kuendesha kozi za madaktari pamoja na kuendeleza mpango wake wa kuinua soka la vijana,ili taifa liwe na wachezaji wenye uwezo wa kushindana na mataifa mengine.

Kasongo amesema licha ya chama chake kuwa na mikakati ya kuhakikisha soka la mkoa wa Dar es salaam na nchi kwa ujumla linanyanyuka,lakini bado nguvu kumbwa inahitajika kutoka Tff pamoja na wadau wenye mapenzi mema na mpira wa nchi hii.

No comments:

Post a Comment