KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, September 11, 2015

TFF, AZAM ZAREJESHA KOMBE LA SHIRIKISHO



Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kwa udhamini wa kampuni ya Azam Media kupitia Azamtv Sports leo wamezindua kombe la Shirikisho litakalofahamika kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) ambalo litaanza kutimua vumbi mwezi Novemba mwaka huu kwa kushirikisha timu 64 nchini.

Kurudishwa kwa michuano hii imekua ni faraja kwa wapenzi na wadau wa mpira miguu nchini baada ya kukosekana kwa takribani miaka 13 michuano hiyo, ambapo sasa Bingwa wa kombe la Shirikisho ataiwakilisha nchi katika michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAFCC).

Akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzindizi wa michuano hiyo na kuchezeshwa droo ya awali, Rais wa TFF Jamal Malinzi amemshukuru Mkurugenzi wa Azam Media Rhys Thorrington kwa kuweza kudhamini michuano ambayo itongeza ushindani zaidi nchini.

Malinzi amesema anaviomba vilabu vitakavyoshiriki michuano ya kombe la hilo, vionyeshe ushindani mkubwa kwani ndio nafasi pekee ya kuweza kuitangaza na kuonekana kwa kuwa michuano hiyo itakua ikionyeshwa moja moja na luninga ya Azamtv.

Aidha Malinzi amesema kila timu inayoshiriki michuano hiyo itapata fedha ya usafiri shilingi milioni 3, na vifaa vitakavyotolewa na mdhamini kampuni ya Azam Media.

Naye Mkurugenzi wa Azam media Rhys Thorrington amesema uhdmaini huo wa miaka mine una thamani ya fedha za kitanzania bilioni 3.3  ambapo timu zitakazoshiriki michuano hiyo zitapata nafasi ya kuonekana moja moja katika nchi zaidi ya saba barani Afrika kupitia kituo chao cha azamtv.

Mshindi wa Kombe la ASFC linalodhaminiwa na kampuni ya Azam kupitia Azamtv Sports, atajinyakuliwa kitita cha shilingi milioni hamsini (TZS 50,000,000), jumla ya timu 64 kutoka Ligi Kuu (VPL), ligi daraja la kwanza (FDL) na ligi daraja la pili (SDL) zitashirki katika kombe hilo.

Timu zote 24 za ligi daraja la pili na 8 za ligi daraja la kwanza 3, zilizopanda daraja na 5 zilizoshika nafasi za chini kwenye makundi yote zitashiriki katika raundi ya kwanzamwezi Novemba kwa kucheza mechi 16 na kupata washindi 16 ambao wataingia raundi ya pili.

Timu 16 zilizoshinda raundi ya kwanza na 16 zilizofanya vizuri ligi daraja la kwanza zitachanganywa na kupangwa kucheza mechi 16 nyingine za raundi ya pili mwezi Desemba.

Washindi wa raundi ya pili wataingia raundi ya tatu ambapo watachanganywa na timu 16 zilizopo ligi kuu na kuchezwa mechi 16 nyingine ambazo washindi wake wataingia raundi ya nne. Raundi hii ya tatu itafanyika mwezi Januari 2016.

Timu 16 zilizoshinda raundi ya tatu zitaingia raundi ya nne zitapangwa ili kucheza hatua hii ambayo itakuwa na mechi  8 na washindi 8 wataingia katika hatua inayofuata ambayo ni raundi ya tano au robo fainali. Raundi hii ya nne itachezwa Februari 2016.

Washindi wa raundi ya nne watapata nafasi ya kuingia raundi ya 5 ambayo pia ni robo fainali, droo itapangwa. Raundi hii ya tano itachezwa mwezi Machi 2016.

Washindi wa raundi ya tano au robo fainali watapangwa kucheza nusu fainali au raundi ya 6 mwezi Aprili.

Washindi wa nusu fainali watapambana katika fainali na kumpata bingwa wa Azam Sports Federation Cup 2015/16. Mechi ya fainali itachezwa wiki moja baada ya ligi kuu kumalizika na Bingwa atakabidhiwa kombe na zawadi ya fedha tasilimu shilingi milioni 50.

Mechi za raundi ya kwanza na raundi ya pili kama mshindi hatapatikana ndani ya dakika 90 basi mshindi atapatikana kwa kupigiana penati moja kwa moja. Mechi za raundi ya tatu na nne kama mshindi hatapatikana ndani ya dakika 90 mechi itarudiwa katika uwanja wa timu iliyokuwa mgeni mechi ya awali.

Mechi za robo fainali au raundi ya tano kama mshindi hatapatikana ndani ya dakika 90 hatua ya penati tano tano itaamua mshindi.

Kwa mechi za nusu fainali na fainali kama mechi itaisha kwa sare ndani ya dakika 90, dakika 30 za nyongeza zitachezwa, na kama hakutakuwa na mshindi penati zitaamua mshindi.

Ratiba ya raundi ya kwanza:

AFC -Arusha Vs Polisi Mara, Polisi -Tabora Vs Green Worries -Dar es salaam, Karikoo Lindi Vs Changanyikeni -Dar es salaam, Mkamba Rangers –Morogoro Vs Mvuvuma - Kigoma, Rhino Tabora Vs Allicane - Mwanza, Panone Kilimanjaro Vs Coca Cola Mbeya, Polisi Morogoro Vs Mshikamo Dar es salaam, Sabasaba Morogoro Vs Abajalo Tabora.

Magereza Iringa Vs Polisi Dar es salaam, Milambo Tabora Vs Town Small Ruvuma, Abajalo Dar es salaam Vs Transit Camp Dar es salaam, Ruvu Shooting Vs Cosmopolitan Dar es salaam, JKT Rwamkoma Mara Vs Villa Sqaud (Dar es salaam), Wenda FC Mbeya Vs Madini Arusha, Pamba FC Mwanza Vs Polisi Dom, Singida United Vs Bulyanhulu FC Shinyanga.

No comments:

Post a Comment