KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, May 2, 2015

SIMBA, AZAM KUVAANA KESHO LIGI KUU





Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara inatarajiwa kuendelea mwishoni mwa wiki hii kwa michezo sita kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini, huku michezo mitatu ikichezwa siku ya Jumamosi na michezo mingine mitatu ikichezwa siu ya jumapili.

Jumamosi katika Uwanja wa Sokoine wapinzani wa jiji la Mbeya, Prisons FC watakuwa wenyeji wa wagonga nyundo Mbeya City mchezo utaochezwa majira ya saa 10 kamili kwa saa za Afrika mashariki na Kati.

Katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona wenyeji timu ya Ndanda SC watawakaribisha wakata miwa wa Kagera Sugar, huku jijini Tanga Mgambo Shooting wakiwa wenyeji wa maafande wa JKT Ruvu mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani.

Jumapili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaa, Simba SC watawakaribisha Azam FC, mchezo ambao unatabiriwa kuwa na upinzani mkali kusaka nafasi ya pili ili mwakani kuweza kuwakilisha Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Jijini Tanga wagosi wa kaya Coastal Union watawakaribisha timu ya Stand United kutoka mjini Shinyanga, mchezo utakaochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani, huku kwenye Uwanja wa Manungu mjini Morogoro wenyeji Mtibwa Sugar wakiwakaribisha maafande wa Ruvu Shooting.

No comments:

Post a Comment