KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, May 17, 2015

MKUTANO MKUU WA WANACHAMA COASTAL UNION LEO



MKUTANO Mkuu wa Dharura wa Wanachama wa Klabu ya Coastal Union
unatarajiwa kufanyika leo kwenye ukumbi wa Bwalo la
Polisi Mkoani Tanga.

Sababu za Mkutano huo kufanyika katika Ukumbi la Polisi Mesi ni
kutokana na makao makuu ya klabu ya Coastal Union kuendelea mchakato
wa uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa na upigaji picha wananchi
kwa ajili ya vitambulisho hivyo.

Akizungumza leo,Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga  alisema
maandalizi ya mkutano huo yanaendelea vizuri na unafanyika kufuatia
vikao vya maridhiano ya Uhakikiwa wanachama wa Klabu ya Coastal Union
ulioongozwa na Mjumbe wa Kamati
ya Utendaji ya Shirikisho la soka nchini (TFF) Ahmed Iddi Mgoyi.

Ambapo alisema  baada ya kumalizika vikao hivyo,Katibu Mkuu wa TFF,
Mwesigwa Selestine aliiandikia barua Klabu ya Coastal Union akiiagiza
klabu hiyo kuitisha mkutano mkuu wa dharura wa wanachama tarehe 17 Mei
mwaka 2015.

Alisema kuwa matokeo  ya maamuzi haya yamepatikana baada ya kikao cha
usuluhishi cha amani kilichoongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya
TFF, Ahmed Iddi Mgoi aliyekuwa ameongozana na Makamu Mkurugenzi wa
Sheria na Uanachama shirikisho la soka nchini (TFF) Eliud Peter Mvella
kilichofanyika April 13 mjini hapa.

Aidha alisema kuwa tayari shirikisho la soka nchini (TFF) ilishatuma
orodha tatu za majina Wanachama stahiki,Wanachama waliobainika kuwa
wanadosari na inabidi wathibitishwe na wanachama stahiki.

Orodha nyengine ni waombaji wapya wa  wa uanachama watakaohakikiwa na
wanachama stahiki ambapo utaratibu huo ndio ulioagizwa kutumika .

Hata hivyo alisema kuwa orodha zote zimekwisha kubandikwa kwenye ubao wa
Matangazo wa Klabu ya Coastal Union tayari kwa ajili ya mkutano huo wa
kesho(leo)

No comments:

Post a Comment