KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, May 10, 2015

POLISI MORO, RUVU SHOOTING ZASHUKA DARAJA

 MICHUANO ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara, ilimalizika rasmi jana kwa mechi saba zilizochezwa kwenye viwanja tofauti, huku ikishuhudiwa timu za Polisi Moro na Ruvu Shooting zikishuka daraja baada ya kupoteza mechi zao.

Ruvu Shooting ilishuka daraja baada ya kupokea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Stand United katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga wakati Polisi Moro ilichapwa idadi hiyo ya bao na Mbeya City kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Tayari timu za Majimaji ya Songea, Toto Africans ya Mwanza na African Sports ya Tanga, zimeshapata tiketi ya kucheza ligi mkuu msimu ujao, ambayo sasa itakuwa na timu 16 badala ya 14.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa jana, Mgambo iliyokuwa kwenye wakati mgumu ilitoka suluhu na Azam kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam, wakati Prisons na Kagera Sugar zilitoka suluhu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Mabingwa wapya wa ligi hiyo, Yanga walipoteza mechi yao ya mwisho kwa kuchapwa bao 1-0 na Ndanda kwenye Uwanja wa Nang'wanda mjini Mtwara, Mtibwa Sugar ilichapwa bao 1-0 na Coastal Union mjini Morogoro.

No comments:

Post a Comment