KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 6, 2015

WAAMUZI WA KIKE WA TANZANIA WAULA


Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika - CAF limewateua waamuzi wa kike kutoka Tanzania kuchezesha mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia kwa Wanawake U-20 mwaka 2016 kati ya Congo DR dhidi ya Gabon.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa jumamosi tarehe 09.05.2015 jijini  Kinshasa - Condo DR, mwamuzi wa kati ni Jonesia Rukya, akisaidiwa na washika vibendera Dalila Jafari na Sophia Mtongoli huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Hellen Mduma.

Wakati huo huo Elizabeth Kalinga ameteuliwa kuwa kamisaa wa mchezo kati ya Kenya dhidi ya Botswana kuwania kufuzu kwa michuani ya Olympiki, mchezo utakaofanyika Mei 31, 2015 nchini Kenya.


NB: Alhamisi ya tarehe 07 Mei, 2015, saa 5 kamili asubuhi, Kocha Mkuu wa timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) Mart Nooij ataongea na waandishi wa habari katika Ukumbi wa mikutano wa TFF uliopo Karume, waandishi wote wa habari mnaombwa kuhudhuria bila kukosa.

No comments:

Post a Comment