KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, May 10, 2015

TFF YAKUBALI UENYEJI KOMBE LA KAGAME


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), leo hii imekubali kuwa wenyeji wa  michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, ngazi ya klabu maarufu kama Kombe la Kagame.


Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), ambalo ndio wamiliki wa mashindano haya, watatoa mialiko kwa klabu zenye sifa ya kushiriki.

Taarifa iliyotolewa na TFF leo mchana imeeleza kuwa, michuano hiyo inatarajiwa kuafanyika nchini kuanzia Julai 11 hadi Agosti 2,  2015.

No comments:

Post a Comment