KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, May 2, 2015

TFF YAIAMURU SIMBA KUWALIPA TAMBWE NA CHANONGO








SIMBA WATAKIWA KUMLIPA CHANONGO MIL 11
Klabu ya Simba SC inatakiwa kumlipa mchezaji Haruni Chanongo sh. 11,400,000,  kufikia Aprili 30, 2015 vinginevyo Sekretarieti ya TFF itaanza kukata mapato ya Simba ili kumlipa mchezaji huyo. 
Iwapo Simba itakuwa na vielelezo vingine katika kikao kinachofuata cha Kamati kitakachofanyika Mei 3, 2015 itafanywa hesabu na Simba kurejeshewa fedha itakayokuwa imezidi.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF imeagiza kwa klabu ya Simba na klabu nyingine zote kuwa kwa wachezaji wa mkopo, maslahi yao (mishahara na posho) yote yailipwe na klabu husika kwa klabu ambayo mchezaji anakwenda kwa mkopo ili malipo yake yawe yanafanyika kutoka kwenye klabu moja badala ya kufuatilia malipo yake katika klabu mbili tofauti, hali hii inaweza msabababishia usumbufu mchezaji aliye kwenye mkopo.

Amissi Tambwe vs Simba Sports Club
Mchezaji Amissi Tambwe aliwasilisha malalamiko dhidi ya Simba ya kutolipwa dola 7,000 za Marekani zilizotokana na klabu hiyo kuvunja mkataba wake Desemba 15, 2014. Uamuzi wa kuvunja mkataba ulikuwa ni wa makubaliano ya pande zote ambapo Simba ilitakiwa iwe imemlipa fedha hizo mlalamikaji kufikia Desemba 17, 2014.

Katibu Mkuu wa Simba SC , Steven Ally alikiri klabu yake kudaiwa na mchezaji huyo na kuwa wameshafanya mawasiliano na wakili wake aliyepo Ureno, Felix Majani na kupanga utaratibu wa kulipa isipokuwa kinachosubiriwa ni kusaini hati ya makubaliano ya malipo (Deed of Settlement).

Kamati imesikitishwa na klabu ya Simba kushindwa kumlipa mchezaji huyo kama ilivyokuwa katika makubaliano ya kuvunja mkataba yaliyofikiwa na pande zote mbili Desemba 15, 2014.

Klabu ya Simba inatakiwa kumlipa Amissi Tambwe fedha hizo kwa awamu mbili. Awamu ya kwanza ya dola 5,000 malipo yawe yamefanyika kufikia Aprili 30, 2015. Salio la dola 2,000 ili kukamilisha jumla ya dola 7,000 liwe limelipwa kufikia Mei 10, 2015, uamuzi ambao upande wa Simba ulikubaliana nao.


Amiri S. Msumi vs Ndanda SC
Klabu ya Ndanda SC imeamuriwa kumlipa mchezaji Amiri S. Msumi kiasi cha fedha sh. 2,600,000. Pia Kamati ilihoji mkataba kutokuwa na kipengele cha mshahara, na kusema ni lazima mkataba uonyeshe Kaiser ambacho mwajiriwa analipwa.

Pia Kamati imeagiza kuwa vilabu vifahamishwe kuwa fedha ya kusaini mkataba (sign on fee) hazitakiwi kulipwa kwa mafungu. Tafsiri ya fedha ya kusaini, ni mchezaji kulipwa fedha yote baada ya kusaini, na si kwa mafungu. Pamoja na uamuzi huo, Katibu Mkuu wa Ndanda SC ametakiwa kuwepo kwenye kikao cha Mei 3, 2015.


Malalamiko mengine yataendelea kusikilizwa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji Mei 3, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment